Home » » RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE KUFUNGUA BARABARA YA TANGA – HOROHORO (KM 65.14) TAREHE 13 APRIL, 2013

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE KUFUNGUA BARABARA YA TANGA – HOROHORO (KM 65.14) TAREHE 13 APRIL, 2013

Wizara ya Ujenzi inapenda kutoa taarifa kwa umma kwamba, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete atakuwa Mgeni Rasmi katika sherehe za ufunguzi wa barabara ya Tanga – Horohoro ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami ikiwa na urefu wa kilomita 65.14.  Aidha, sherehe hizo zitahudhuriwa na Bw. Daniel Wolde Yohannes, Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Changamoto za Milenia wa Marekani.

Barabara ya Tanga – Horohoro ni sehemu ya barabara inayoiunganisha Tanzania na nchi jirani ya Kenya kupitia mkoa wa Tanga.  Mradi huu umepata msaada wa Serikali ya Marekani kupitia Mfuko wa Changamoto za Milenia (Millennium Challenge Corporation - MCC).

Kukamilika kwa barabara hii ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya Nne ya kuboresha miundombinu muhimu ya usafiri wa barabara.  Aidha, kukamilika kwa barabara hii kutapanua fursa za kibiashara kati ya Tanzania na Kenya na hivyo kutumia vizuri zaidi fursa za Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Sherehe hizi zitafanyikia kijiji cha Kisera katika Wilaya ya Nkinga mkoani Tanga.


Taarifa hii imetolewa na;


Balozi Herbert E. Mrango KATIBU MKUU

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa