Home » » ‘SERIKALI IHAMISHE WANAOISHI HIFADHI YA SAADANI’

‘SERIKALI IHAMISHE WANAOISHI HIFADHI YA SAADANI’

na Bertha Mwambela, Pangani
MKUU wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani, Hassan Nguluma, ameiomba serikali kuwasaidia kuwahamisha wananchi waishio vijiji vilivyopo jirani kutokana na ongezeko la kasi la uzalianaji wa wanyama hifadhini hapo, hali inayotishia usalama wao.
Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea hifadhi hiyo mwishoni mwa wiki, Nguluma alisema kumekuwa na ongezeko kubwa la wanyama kuzaliana, hivyo kufanya eneo la hifadhi kuwa dogo.
“Tunaomba serikali itusaidie kuwahamisha wananchi walio jirani na hifadhi, ili tuweze kupata nafasi ya kutosha kwa ajii ya shughuli za uhifadhi, kwani kwa sasa kumekua na ongezeko kubwa la wanyama,” alisema Nguluma.
Kwa upande wake, mkazi wa Kijiji cha Saadani kilichopo jirani na hifadhi hiyo, Rished Mwinyibabu, alisema anaona kuwa kuna faida kubwa kuwepo kwa hifadhi jirani na wao kwani hata wale wanyama waliopotea wakati lilipokuwa pori la akiba kwa sasa wamerudi baada ya kupandishwa hadhi na kuwa hifadhi ya taifa.
Chanzo: Tanania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa