Home » » WAKAZI TANGA KUTUMIA STENDI YA KANGE

WAKAZI TANGA KUTUMIA STENDI YA KANGE

 Stendi ya Kange
 WAKAZI wa Jiji la Tanga wametakiwa kukitumia kituo kipya cha mabasi yaendayo mikoani na wilayani kilichopo Kange ingawa
bado kuna baadhi ya changamoto za kukamika kwake.
Rai hiyo ilitolewa na Mstahiki Meya wa Jiji hilo, Omary Gulledy alipozungumza na madiwani katika kikao cha baraza kilichofanyika jijini hapa.
Alisema wakazi wa Tanga wasione kimya katika umaliziwaji wa kituo hicho bali ni serikali inaendelea na mchakato wa kufikisha huduma zote muhimu kwenye stendi hiyo mpya.
Sambamba na hayo Gulledy alisema lengo hasa la kuhamishia stendi hiyo Kange ni kulikuza jiji baada ya kituo cha mabasi kilichokuwepo kuwa kidogo.
Kwa upande wake Naibu Meya wa jiji hilo Mzamini Shemdoe alisema kuna mipango ya muda mfupi na mrefu kwa ajili ya kujenga vibanda vya biashara vya muda ili kukidhi mahitaji ya wasafiri na wakazi kwa ujumla.

 Chanzo;Tanzania Daima
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa