Home » » MAMIA WAMZIKA MKE WA MWANDISHI WA HABARI WA GAZETI LA MWANANCHI MKOANI TANGA

MAMIA WAMZIKA MKE WA MWANDISHI WA HABARI WA GAZETI LA MWANANCHI MKOANI TANGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Sehemu ya waandishi wa habari mkoani Tanga wakiwa nyumbani kwa Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi mkoani Tanga,Burhan Yakub ambaye alifiwa na mkewe wakati wa mazishi ambayo yamefanyika leo Makaburi ya Magomeni Jijini Tanga
Sehemu ya waombolezaji wakiwa wamelibeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mke wa Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi Mkoani Tanga wakilipeleka makaburini tayari kwa ajili ya maziko.
 Sehemu ya waombolezaji wakiwa msibani eneo la Magomeni Jijini Tanga
 Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali Jijini Tanga wakiwa msibani leo katikati mwenye tisheti ya mistari ni Mwandishi Mwandamizi wa ITV na Radio One mkoani Tanga,William Mngazija kulia ni Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Tanga,Hassan Hashim
 Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi Mkoani Tanga,Burhan Yakub kushoto ambaye amefiwa na mkewe akiwa na ndugu jamaa wakati wa msiba huo nyumbani kwake eneo la magomeni Jijini Tanga.
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella akiingia kwenye eneo la Msiba leo
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella katikati akiwa eneo la msibani Magomeni Jijini Tanga kulia ni Katibu Itikadi na Uenezi CCM wilaya ya Tanga,Lupasio Kapange

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella kushoto akisalimiana na wananchi waliokuwepo msibani mara baada ya kuwasili
Wananchi wakifukia mwili wa aliyekuwa mke wa Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Mwananchi mkoani Tanga,Burhan Yakub
 Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu akisalimiana na Katibu wa CCM mkoa wa Tanga,Allan Kingazi wakati wa mazishi hayo
  Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu akisalimiana na Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga,Alhaj Mustapha Selebosi
Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Tanga,Hassan Hashimn akiteta jambo na wandishi wa habari mkoani Tanga wakati wa msiba huo(Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa