Na Benedict Liwenga-MAELEZO, Dodoma.
Wawekezaji
kutoka Sekta Binafsi nchini wenye nia ya kufungua Viwanda vya juisi
mkoani Tanga ikiwemo Wilaya ya Muheza wamehimizwa kuwekeza katika
biashara hiyo mkoani humo.
Hayo
yamesemwa leo na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Charles Mwijage
wakati wa kipindi cha maswali na majibu, ambapo Mhe. Mwijage alikuwa
kijibu swali lililoulizwa na Mheshimiwa Balozi Adadi Mohamed Rajabu,
Mbunge wa Muheza lililotaka kujua ni lini Serikali itajenga kiwanda cha
matunda wilayani hapo na kuwaondolea usumbufu wakulima katika utafutaji
masoko.
Mhe.
Mwijage amesema kuwa tafsiri ya Serikali katika kujenga viwanda ni kwa
serikali kuweka mazingira sahihi na wezeshi ili kuwavutia wawekezaji wa
ndani na nje wa sekta binafsi kujenga viwanda.
Aidha,
aktika kutekeleza hilo Mhe. Mwijage ameeleza kuwa Sera na Mikakati
mbalimbali shirikishi inatoa fursa kwa Sekta na Taasisi za uwekezaji
kujenga viwanda na kunufaika na vivutio mbalimbali.
“Mkoa
wa Tanga ikiwemo Wilaya ya Muheza wamejaaliwa kuwa na utajiri wa
matunda aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na machungwa, maembe, machenza,
mafenesi na mananasi, kwa kutambua upatikanaji wa matunda hayo, Wizara
yangu inahimiza na kuhamasisha wawekezaji kutoka Sekta Binafsi wenye nia
ya kufungua viwanda vya juisi mkoani Tanga wafanye hivo’’, alisema Mhe.
Mwijage.
Amefafanua
kuwa, mpaka sasa Kampuni ya M/s Sasumua Holding imeanzisha mradi mkubwa
wa kulima matunda katika utaratibu utakaoshirikisho wananchi na kufikia
mwezi Novemba, 2018 kiwanda cha juisi kitakuwa tayari kinafanya kazi.
“Mradi
huu uko kwamsisi, Handeni mkoani Tangam hivyo ni tegemo langu kuwa
mafaniko ya Mwekezaji huyo yatawavutia wawekezaji wengine”, alisema Mhe.
Mwijage.
Ameongeza
kuwa, Wizara kupitia Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) ina utaratibu wa
kutoa ushauri jinsi ya kuanzisha mitaa ya viwanda kila mkoa ikiwa ni
jitihada za kuweka mazingira wezeshi kwa sekta binafsi kuendeleza
uzalishaji katika mikoa husika.
0 comments:
Post a Comment