Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.
Samia alisema hayo juzi alipozungumza na viongozi wa CCM kutoka
wilaya zote za mkoa wa Tanga na wabunge wa mkoa huo katika ukumbi wa CCM
jijini Tanga.
Alisema ndani ya chama cha CCM kuna watu ambao ni watendaji wa
serikali ambao hawarekebishiki kwa kuwa wamejificha ndani ya chama ili
kuficha mambo yao.
Alisema kuna watu wamo ndani ya CCM wanafanya biashara lakini
hawalipi kodi ya mapato serikalini. Samia alikemea tabia hiyo na
kuagiza viongozi wa CCM kuwabana watu hao na kuziba mianya ya kukwepa
kodi ili kuongeza mapato ya serikali.
Pia alisema ndani ya chama hicho kuna wanafiki kama mchwa
wanafukuta ndani kwa kuharibu chama na kusababisha watu wagombane.
Aliwataka watu hao wondoke mapema ndani ya chama ili kuendelee kuwa
salama na kuongoza nchi.
Samia aliwatupia 'dongo' wabunge wa mkoa wa Tanga kuwa ni wavivu na
kuwataka wawe wanakwenda kuwatembelea wananchi wao badala ya kukaa tu
mijini.
Alisema kuwa hata kama hawana fedha, waende hivyo hivyo kwa kuwa wananchi watawaelewa lakini si kuingia mitini moja kwa moja.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment