Home » » MISS TANGA 2014 WAFUNDWA

MISS TANGA 2014 WAFUNDWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

KATIKA kuelekea kinyang’anyiro cha kumsaka Nice&Lovely Miss Tanga 2014, washiriki wametakiwa kujiamini na kuongeza juhudi ili waweze kufanya vizuri katika fainali za shindano hilo kwenye ukumbi wa Hoteli ya Mkonge, June 21.
Ushauri huo umetolewa na Miss Tanga 2012, Theresia Kimolo, ambaye alikuwa ni miongoni mwa wapenzi wa tasnia ya urembo mkoani Tanga waliojitokeza kushuhudia mazoezi ya warembo wanaowania taji hilo yanayofanyika kwenye hoteli ya Tanga Beach Resort, chini ya Mwalimu wao Mariam Bandawe.
Alisema, washiriki hao hawana budi kuzidisha uelewa kwenye maeneo mbalimbali, ikiwemo kujieleza, kutabasamu na kutembea mbele za watu, lengo likiwa kuleta ushindani wakati wa maandalizi yao na hata hatua ya kumsaka bingwa wa kinyang’anyiro hicho.Awali, akizungumza mara baada kumalizika mazoezi hayo, Mratibu wa shindano hilo, Benson Jackson alisema, maandalizi ya kuelekea shindano hilo yamekamilika kwa asilimia kubwa. kwa warembo hao kufanya maandalizi kila siku.
 Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa