BAADHI
ya Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Tanga wametaka mashamba ya mkonge
yaliyotelekezwa kwa muda mrefu yagawiwe kwa wananchi ili waweze kulima
na kujenga makazi.
Hayo yalisemwa juzi kwenye maswali ya papo kwa
hapo na Diwani wa Kata ya Marungu, Mohamed Mambea kwenye Baraza la
Madiwani wa Jiji la Tanga na kusema kata yake inamashamba mawili ya
mkonge yaliyotelekezwa, lakini sheria inawabana wananchi kuweza
kuyatumia kwa kilimo.
"Kata ya nguya Marunguku na mashamba mawili ya
mkonge ambayo yamekufa au kushindwa kuendelezwa zaidi ya miaka 20 sasa.
Na sheria ya ardhi inasema, ardhi ikitelekezwa kwa zaidi ya miaka 12 mtu
mwingine akiendeleza ardhi hiyo sheria inamtambua anayo haki.
"Katika
maeneo hayo wananchi wa Kijiji cha Geza, Marungu na Mkembe wamejenga na
kulima kwenye maeneo hayo. Je ni liniyatapelekwa kwa Rais ili kufuta
hati na kuweza kupewa wananchi," alisema Mambea.
Mambea alisema pia
kuna mradi wa maji unaogharamiwa na Benki ya Dunia kwenye vijiji vitano
vya kata vya Marungu , Geza, Kirare, Mapojoni na Mwarongo, lakini mradi
huo unasuasua na hawajui hatima yake .
Naye Diwani wa Kata ya
Msambweni, Abdulraham Hassan Omar alisema Halmashauri ya Jiji imetoa
ardhi yenye thamani ya sh.bilioni 3.5 kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda
eneo la Pongwe, lakini mradi huo ni kama umesimama, kwani hawaoni kitu
kinachoendelea.
"Mradi huu umekuwa unasuasua kwa muda mrefu bila
kuendelezwa. Halmashauri ina utaratibu gani kwa kuzingatia thamani ya
ardhi inapanda siku hadi siku, na utaratibu gani unafanyika kwa
kuzingatia muda na mikataba," alisema Omar.
Akijibu baadhi ya
maswali hayo, Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga, Omar Guledi alisema
mashamba hayo kwa muda mrefu yalikuwa na kesi mahakamani, hivyo ili
kuonekana hayaendelezwi ni lazima hesabu ya miaka ianze baada ya
kumalizika kesi, hivyo bado hayajafikisha miaka ya kufutiwa hati zake.
"Kuhusu
maji Serikali imesema haina fedha, ila kama mkandarasi ataendelea na
ujenzi kwa fedha zake, basi Serikali itakuja kumrudishia," alisema
Guledi.
Naye Mkurugenzi wa Jiji hilo Juliana Malange alisema ni kweli
wameingia mkataba na Kampuni ya Good PM ya Korea kwa ajili ya
uendelezaji wa eneo hilo, lakini mchakato wake bado unaendelea kwani
umehusisha watu wengi ikiwemo Mamlaka ya Uwekezaji Kanda Maalumu (EPZA)
na Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC).
0 comments:
Post a Comment