Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MTOTO wa miaka saba wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi
Mkata wilayani Handeni, Tanga amebakwa na babu yake na kumsababishia
maumivu makali na kumwagika damu nyingi.
Tukio hilo lilibainika wakati mtoto huyo akiwa darasani na wenzake
ambapo alianza kuvuja damu nyingi hali iliyowafanya wanafunzi wenzake
kutoa taarifa kwa Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Moses Kimlayi, aliyefika
kushuhudia tukio hilo.
Baada ya kupewa taarifa hiyo Mwalimu Kimlay alimkabidhi mwanafunzi
huyo kwa walimu wa kike kwa lengo la kumchunguza kama kweli kuna unyama
aliofanyiwa. Baada ya kumhoji mwanafunzi huyo alisema babu yake
alimbaka na kumtishia asimueleze mtu yeyote.
Chanzo:Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment