Askofu wa Kanisa la Aglikana Jimbo la Tanga, Mahimbo Mndolwa
Zaidi ya wanafunzi 460 walivamia na kutaka kuchoma hospitali hiyo.
Wanafunzi hao walikuwa wakisema kuwa wamepata taarifa kwamba kozi hiyo haijasajiliwa wizarani na wala haifahamiki na kwamba fedha zao za ada zimekwenda bure.
Mmoja wa wanafunzi hao ambaye aliomba jina lake listanjwe aliwaambia waandishi wa habari kwamba hapo mwanzo walikuwa wanavaa sare za chuo, lakini cha kushangaza hivi karibuni wamezuiwa wasivae wakidai kuna wakaguzi walifika wakauliza waliyovaa sare zile ni kina nani.
Alisema pia waliambiwa kuwa kozi hiyo itamalizika Aprili mwaka huu, lakini baadaye wakaambiwa kuwa itamalizika Machi, kitu ambacho wanashindwa kuelewa.
Wanafunzi hao walisikika wakisema wanamtaka Askofu wa Kanisa la Aglikana Jimbo la Tanga, Mahimbo Mndolwa, ambaye kanisa lake ndilo linalomiliki chuo hicho kueleza ukweli kuhusu kozi hiyo kama mmoja anaitambua ama la.
Walisema kuwa kama hawataelezwa ukweli, wataandamana hadi kwa mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa na kwa Rais Jakaya Kiwete. Mganga Mfawidhi wa
Hospitali Teule wilayani Muheza, Dk. Rajabu Mlahiyo, hakupatikana kuzungumzia suala hilo kutokana na kuwa safarini kikazi.
Wanafunzi hao wanalipa kozi ya mwaka mmoja Sh. 600,000 na sare wanashona wenyewe.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment