Home » » TAKUKURU Tanga yatakiwa kuchunguza halmashauri

TAKUKURU Tanga yatakiwa kuchunguza halmashauri

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Tanga, wametakiwa kuchunguza ufisadi unaofanyika kwenye halmashauri zote za mkoa huo na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria watakaobainika.
Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa, wakati wa sherehe za kuuaga mwaka 2013 na kuukaribisha mwaka 2014 zilizoandaliwa na taasisi hiyo mwishoni mwa wiki na kueleza kuwa kuna ufisadi unaotendeka kwenye halmashauri hali inayosababisha kudumaza juhudi za maendeleo zinazofanywa na serikali kuu.
Aliitaka TAKUKURU kufanya kazi yake kwa uadilifu ili kuwabaini mchwa wote, hasa watendaji wenye mamlaka waliopo kwa ajili ya kuchota fedha za wananchi kwa manufaa yao.
“Hatuwezi fika tunakokutaka iwapo kuna wachache wetu wanakwamisha jitihada za kujiletea maendeleo kwa ubinafsi na  kupenda kujilimbikizia mali kwa njia isiyo halali ikiwemo rushwa za miradi ya maendeleo,” alisema Gallawa.
Hata hivyo, Kamanda wa TAKUKURU mkoani hapa, Edson Makallo, alisema: “Serikali peke yake haiwezi kumaliza rushwa katika nchi hii bila kushirikisha wadau kama mahakama, polisi na wanasheria. Lazima tuongee lugha moja ya kuhakikisha tunapigania jambo hili kwa uadilifu.”
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa