HALMASHAURI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC-CCM) Mkoa wa Tanga
imekemea tabia ya watendaji wa serikali wanaojifanya miungu watu na
kuzitaka mamlaka husika kuhakikisha wanawachukulia hatua za kisheria
ili kukomesha vitendo hivyo.
Uamuzi huo ulifikiwa juzi wakati wa kikao hicho kilichohudhuriwa na
wajumbe kutoka wilaya zote za mkoa huu, ambapo mambo mawili
yaliyotawala ni migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji na
mgogoro kati ya wakulima wa chai, chama cha wakulima wa chai (Utega) na
mwekezaji.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Katibu wa CCM Tanga, Gustav
Mubba, alisema viongozi wa serikali wanaopewa mamlaka ya kuwaongoza
wananchi wanashindwa kufanya kazi zao ipasavyo na kuendekeza tabia ya
kuwanyanyasa badala ya kuwaondolea kero zao.
Mubba alisema viongozi wa ngazi za chini wameshindwa kuwajibika kwa
kuwa mstari wa mbele kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazowakabili
wananchi bali wanachangia kuwepo kwa migogoro kwenye maeneo yao kwa
kutokuzingatia namna ya utoaji wa ardhi kisheria na kuwafanya wananchi
kuwatupia lawama viongozi wao.
Alisema kitendo hicho kimeleta manung’uniko kwa wananchi wa wilaya za
Kilindi na Handeni, hali iliyowafanya kuichukia serikali yao.
Aidha, katibu huyo alisema kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2014/2015
viongozi wa vijiji, madiwani na wabunge watapimwa kwa kazi walizofanya.
Akizungumzia suala la mgogoro wa wakulima wa chai, chama cha wakulima
na mwekezaji, Mubba alisema halmashauri hiyo imeunda kamati ya watu
saba kuonana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ili kuangalia namna sahihi
ya kumaliza mgogoro huo.
CCM Tanga yawakemea viongozi miungu watu
HALMASHAURI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC-CCM) Mkoa wa Tanga
imekemea tabia ya watendaji wa serikali wanaojifanya miungu watu na
kuzitaka mamlaka husika kuhakikisha wanawachukulia hatua za kisheria
ili kukomesha vitendo hivyo.
Uamuzi huo ulifikiwa juzi wakati wa kikao hicho kilichohudhuriwa na
wajumbe kutoka wilaya zote za mkoa huu, ambapo mambo mawili
yaliyotawala ni migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji na
mgogoro kati ya wakulima wa chai, chama cha wakulima wa chai (Utega) na
mwekezaji.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Katibu wa CCM Tanga, Gustav
Mubba, alisema viongozi wa serikali wanaopewa mamlaka ya kuwaongoza
wananchi wanashindwa kufanya kazi zao ipasavyo na kuendekeza tabia ya
kuwanyanyasa badala ya kuwaondolea kero zao.
Mubba alisema viongozi wa ngazi za chini wameshindwa kuwajibika kwa
kuwa mstari wa mbele kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazowakabili
wananchi bali wanachangia kuwepo kwa migogoro kwenye maeneo yao kwa
kutokuzingatia namna ya utoaji wa ardhi kisheria na kuwafanya wananchi
kuwatupia lawama viongozi wao.
Alisema kitendo hicho kimeleta manung’uniko kwa wananchi wa wilaya za
Kilindi na Handeni, hali iliyowafanya kuichukia serikali yao.
Aidha, katibu huyo alisema kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2014/2015
viongozi wa vijiji, madiwani na wabunge watapimwa kwa kazi walizofanya.
Akizungumzia suala la mgogoro wa wakulima wa chai, chama cha wakulima
na mwekezaji, Mubba alisema halmashauri hiyo imeunda kamati ya watu
saba kuonana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ili kuangalia namna sahihi
ya kumaliza mgogoro huo.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment