Home » » Sasa ni Siasa au?: CUF NA BANGO LA MAITI YA MGOMBEA WA CCM - Maeneo ya kata ya Msambweni hapa jijini Tanga

Sasa ni Siasa au?: CUF NA BANGO LA MAITI YA MGOMBEA WA CCM - Maeneo ya kata ya Msambweni hapa jijini Tanga






Taarifa  zilizo na mahusiano na  picha hapo juu  zilizokutwa maeneo ya  kata ya Msambweni  mjini Tanga.  Wanachama wa CUF waliamua kutumia jeneza bandia na kinyago cha maiti kuonyesha hisia zao za kufurahia ushindi wa kata hiyo walio upata kwenye uchaguzi uliofanyika huko. sidhani kama ni vizuri tukifikia huku! Ushabiki wa namna hii unaweza kuleta chuki na madhara, ni haki yao CUF kuonyesha  furaha yao ila kwa jinsi hii haipendezi! kuweka picha ya mgombea wa CCM aliyeshindwa kwenye uchaguzi kwenye mfano wa jeneza bandia tena huku wakiweka sania ambalo kila anae pita njia anatupia pesa kama rambirambi  haipendezi na sidhani kama ushabiki huu unafundisha kitu.

Kwa Tukio zaidi ingia hapa: CHINGA ONE BLOG

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa