Home » » TANGA YATAJA VITUO 3 VYA KUDHIBITI EBOLA

TANGA YATAJA VITUO 3 VYA KUDHIBITI EBOLA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

MKOA wa Tanga umetenga vituo kadhaa vya afya vitatu, ikiwa ni hatua ya maandalizi ya kudhibiti watu watakaobainika kuambukizwa virusi vya homa ya ebola.
Vituo hivyo ni cha kwenye mpaka wa Horohoro wilayani Mkinga, Masiwani Shamba na Maramba. Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa alibainisha hayo juzi katika mkutano na waandishi wa habari.
Alisema timu maalumu ya mkoa ya wataalamu wa afya, tayari inakagua uwezo wa vituo vingine vilivyotengwa na halmashauri nyingine za mkoa huo, kama vinastahili kupokea wagonjwa wa aina hiyo.
Alisema ingawa mpaka sasa hakuna mgonjwa wa ebola nchini, serikali imechukua hadhari hiyo, kuwaondoa wasiwasi wananchi kutokana na mwingiliano wa wageni kutoka nchi jirani kupitia mpaka wa Horohoro.
Alisema vituo hivyo vitatu vimeimarishwa kwa kupelekewa vifaa tiba, madaktari na wauguzi wenye stadi za kutosha na vitatumika kutoa huduma kwa wagonjwa watakaobainika.
“Kwa kuwa ebola haina chanjo wala tiba, mpango mkakati wa mkoa sasa ni kuhakikisha wananchi wanaelimishwa kuhusu namna ya kujikinga kuzuia maambikizi…pia tumeziagiza halmashauri zote 11 zinazounda mkoa kutenga maeneo sahihi ya kupokelea wagonjwa hao”, alisema.
Aliongeza, “wananchi ondoeni wasiwasi na tunawataka muimarishe usafi wa mazingira, hakikisheni mnanawa vizuri mikono kwa maji safi na sabuni…acheni kusalimia kwa kushikana mikono na watu kila mahali”, alisema.
Chanzo;Habari Leo

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa