Home » » WALIMU WALIOJIONGEZEA MADAI KUKIONA CHAMOTO

WALIMU WALIOJIONGEZEA MADAI KUKIONA CHAMOTO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
SERIKALI imesema itawachukulia hatua walimu wote waliojiongezea madai kwa udanganyifu na kuahidi kuwalipa wale wote wenye madai halali.
Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Hawa Ghasia wakati wa ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe.
Alisema baadhi ya walimu wamekuwa wakifanya udanganyifu kwa kujiongezea kiwango cha madai yao kwa serikali, tofauti na madai yao halali.
Waziri Ghasia alisema tabia  hiyo imekuwa ikiikera serikali, kwani wanachangia kwa kiasi kikubwa kulisababiashia hasara taifa, hali itakayochangia kurudi nyuma uchumi.
“Walimu tekelezeni wajibu wenu, kwani mpo hapa kwa ajili ya kutoa huduma bora na stahiki kwa jamii na si kufanya utapeli,” alisema Ghasia.
Awali, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Lewis Kalinjuna, alisema wanatekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.
Kalinjuna alisema baadhi ya miradi waliyotekeleza ni ujenzi wa maabara tatu za sayansi katika kila shule ya sekondari pamoja na kuboresha miundombinu ya maji na afya
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa