Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Wananchi waishio maeneo mbalimbali katika Jimbo la Bumbuli wilayani Lushoto mkoani Tanga wamempongeza Mbunge wa Bumburi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba kwa hatua ya kuwasaidia kuishawishi serikali kukipatia ufumbuzi mgogoro wa kiwanda cha chai cha Mponde.
Wnanchi wakimpongeza Mbunge wa Bumburi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba
NA RAISA SAIDI, BUMBULI.
SERIKALI ya Tanzania imevunja rasmi mkataba na mwekezaji
wakiwanda cha kuzalisha Chai cha Mponde kilichopo wilayani Bumbuli
Mkoani Tanga na kuamuru kitwaliwe na kianze kazi mara moja.
Akizungumza katika mkutano uliowajumuisha wadau wazao la
chai,Msajili wa Hazina Laurence Mafuru amesema kuwa kwa mamlaka
aliyopewa amevunja rasmi mkataba huo kwasababu Mwekezaji
aliyekuwepo kashindwa kutekeleza makubaliano yaliyoweka .
Mafuru alisema kuwa wamefikia uwamuzi huo kutokana na
kujiridhisha pamoja na kupitia mikataba walioingia na mwekezaji
huyo ndipo serikali imeamua ikirudishe kiwanda hicho mikononi
mwa Wizara ya Viwanda na Biashara ili utaratibu mpya wa
uendeshwaji wa kiwanda uanze huku Bodi ya Chai Tanzania
ukiendelea kukisimamia mpaka hapo serikali itakapotafuta mwekezaji
mwingine.
Mei mwaka 2013, wakulima wa chai waliitisha mkutano na kumwalika
Mbunge wa Jimbo la Bumbuli Januari Makamba na kueleza kutokuwa na
imani na mwekezaji na Chama cha Wakulima wa Chai cha Usambara (UTEGA)
na kuamua kukifunga kiwanda licha ya Mbunge kuwasihi wasichukue uamuzi
huo wa hasira.
Tangu wakati huo jitihada nyingi zimefanyika zikiongozwa na Mheshimiwa
Makamba kuhakikisha kwamba kiwanda kinafunguliwa na wakulima wanauza
chai yao.
"Tuliteseka kwa muda mrefu na leo Serikali imefanya uamuzi
wa kukirudisha kiwanda mikononi mwetu, Tunaishukuru Serikali kwa
kutusaidia sisi wananchi tulioteseka kwa muda mrefu ,” Alisema
Challes Ngovi ambaye ni mkulima wa chai Mponde.
Hata hivyo Mafuru alibainisha kuwa ucheleweshaji wa kukifungua
kiwanda hicho ulitokana na utaratibu uliokuwa ukifanywa na Serikali
na baada ya kujiridhisha ndipo ikaamua kumuandikia rasmi
barua Mwenyekiti wa Utega inayoonyesha kuvunjwa kwa mkataba huo
na kuamuru kiwanda kirudi Serikalini.
Kwa upande wake, Mbunge wa Bumbuli January Makamba alisema kwamba
kazi waliyomtuma wananchi ya kukirudisha kiwanda mikononi mwao
imekamilika ingawa imechukua muda mrefu.
Makamba ambaye pia ni Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais
anayeshughuliokia Mazingira na Muungano alitumia nafasi hiyo
kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Magufuli kwa
kuingilia kati mgogoro huo ambao umedumu kwa zaidi miaka mitatu
na hatimae kuumaliza.
Wakati huo huo,Wananchi waishio maeneo mbalimbali katika Jimbo la
Bumbuli wilayani Lushoto mkoani Tanga wamempongeza Waziri wa Nchi
Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira kwa
hatua ya kuwasaidia kuishawishi serikali kukipatia ufumbuzi mgogoro wa
kiwanda cha chai cha Mponde.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi wa habari hizi, mmoja ya
wakulima hao,Swahiba Mbili alisema kuwa kufunguliwa utawasaidia
wananchi ambao walikuwa na changamoto ya mazao yao kuharibika shambani
kupata soko la uhakika ambalo linaweza kuwainua kimaisha.
Swahiba alisema kuwa wao kama wakulima pamoja na kuishukuru serikali
kutwaa kiwanda lakini wanamshukuru Januari Makamba kwa sababu hakuweza
kuwa mbali nao kwenye kipindi chote wakati kiwanda hicho kimefungwa na
kuaidi kumpa ushirikiano katika kipindi cha kuwatumikia wananchi hao.
0 comments:
Post a Comment