Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Shehena ya bidhaa mbalimbali yenye thamani ya
mamilioni ya Shilingi ikiwemo vipuri vya magari kutoka nchini tofauti
zimekamatwa katika bandari bubu ya Kigombe iliypo wilayani Muheza Mkoani
Tanga wakati ikiingizwa nchini Kinyume cha Sheria.
Kaimu Kamanda mkoa wa Tanga mrakibu mwandamizi wa Jeshi la Polisi Mayala Towo
Akizungumza
katika eneo la tukio Kaimu Kamanda mkoa wa Tanga mrakibu mwandamizi wa
Jeshi la Polisi Mayala Towo amesema shehena hiyo ilikua pia na mafuta ya
kupikia kutoka ubelgiji,Sukari kutoka India na vipuri kutoka nchi
tofauti za Ulaya.
Kwa upande wake meneja wa mamlaka ya mapato nchini (TRA) tawi la Tanga Bwana Samir Buelgaaba amekiri kuwa hali ya ukwepaji wa kodi katika bandari bubu ya Kigombe ni ya kutisha kwa sababu sehemu kubwa ya bidhaa zinazouzwa katika maduka mbalimbali katika baadhi ya maduka yaliyopo katika jiji la Tanga, Muheza na Mkinga zinatoka nje ambazo inadaiwa kuwa zimeingizwa nchini kinyume cha sheria.
Kufuatia hatua hiyo kaimu meneja wa forodha mkoa wa Tanga Bwana Jumbe Magoti amesema wazingatia sheria zilizowekwa katika zoezi la tozo za faini kisha watataifisha vyombo vilivyotumika katika usafirishaji wa bidhaa hizo kutoka kisiwani Zanzibar kuingizwa bara bila kulipiwa ushuru.
Chanzo: East Africa Tv
Kwa upande wake meneja wa mamlaka ya mapato nchini (TRA) tawi la Tanga Bwana Samir Buelgaaba amekiri kuwa hali ya ukwepaji wa kodi katika bandari bubu ya Kigombe ni ya kutisha kwa sababu sehemu kubwa ya bidhaa zinazouzwa katika maduka mbalimbali katika baadhi ya maduka yaliyopo katika jiji la Tanga, Muheza na Mkinga zinatoka nje ambazo inadaiwa kuwa zimeingizwa nchini kinyume cha sheria.
Kufuatia hatua hiyo kaimu meneja wa forodha mkoa wa Tanga Bwana Jumbe Magoti amesema wazingatia sheria zilizowekwa katika zoezi la tozo za faini kisha watataifisha vyombo vilivyotumika katika usafirishaji wa bidhaa hizo kutoka kisiwani Zanzibar kuingizwa bara bila kulipiwa ushuru.
Chanzo: East Africa Tv
0 comments:
Post a Comment