Home » » SHENGELA AWATOA HOFU WANANCHI BOMBA LA MAFUTA

SHENGELA AWATOA HOFU WANANCHI BOMBA LA MAFUTA

Shigela awatoa hofu wananchi bomba la mafuta

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela

SERIKALI imewaondoa hofu wananchi ambao maeneo yao ya ardhi, yatatumika kutekeleza mradi wa ujenzi wa Bomba la Mafuta ghafi la Afrika Mashariki (EACOP).
Bomba hilo linaanzia nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga kwamba sheria itazingatiwa ili kila mmoja aweze kulipwa fidia inayostahili.
Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela wakati wa ziara fupi katika Kata ya Chongoleani. Alitembelea eneo hilo ili kukagua eneo la ujenzi wa gati ambalo litatumika kupokea mafuta hayo ghafi kabla ya kusafirishwa kwenda kwenye masoko ya kimataifa.
Alisema mpaka sasa mchakato wa utekelezaji mradi huo, unaokadiriwa kugharimu zaidi ya Sh bilioni 4, unakwenda vizuri na kwamba wakati watendaji wakisubiri muongozo utakaopitishwa kuhusu namna ya ulipaji wa fidia kwa baadhi ya wananchi wa maeneo ya nchi za Tanzania na Uganda.
Mkoa wa Tanga umeanza kujiandaa kwa kusafisha eneo pamoja na miundombinu ya barabara ili kuwezesha vifaa kufika kwa urahisi katika eneo la ujenzi.
Kwa upande wake, Kaimu Kamishna Msaidizi anayeshughulikia masuala ya Petroli katika Wizara ya Nishati na Madini, Mwanaamani Kidaya alisema ameridhishwa na maandalizi ya awali yaliyofanywa na uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga.
CHANZO: GAZETI LA HABARI LEO
 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa