Wananchi
wa Pangani/Bweni mkoani Tanga wamepata kivuko kipya cha MV. Tanga,
ambacho sasa kitasaidiana na MV. Pangani II kutoa huduma katika eneo la
Pangani/Bweni.
MV.
Tanga iliwasili Pangani siku ya ijumaa saa moja jioni, ikitokea katika
bandari ya Dar es salaam ambako ndiko ujenzi wake ulifanyika. Ujenzi wa
kivuko cha MV. Tanga umefanywa na Kampuni ya kitanzania iitwayo Songoro
Marine Company Ltd.
Akiongea
na wananchi wa Pangani Naibu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi kutoka
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Lazaro Vazuri alisema
kuwa kukamilika kwa ujenzi wa kivuko kipya cha MV. Tanga ni muendelezo
wa sera ya Serikali ya kuboresha huduma kwa wananchi wake.
Nae
Mtendaji Mkuu TEMESA Mhandisi Lekujan Manase alisema “TEMESA imejipanga
kuhakikisha kuwa vivuko vyake vyote vinafanyiwa matengenezo ya kinga
kwa wakati, ili kuhakikisha kuwa huduma kwa wananchi wanaotumia vivuko
hivyo inapatikana kwa wakati muafaka hivyo MV. Pangani II sasa itakwenda
kwenye ukarabati na baada ya ukarabati huo vivuko vyote viwili
vitabakia katika eneo la Pangani/Bweni ili kuendelea kutoa huduma kwa
wananchi.”
Wananchi
wa Pangani/Bweni wamekipokea kivuko cha MV. Tanga kwa furaha kubwa na
kuiomba Serikali kutoa huduma ya kivuko kwa saa 24 kwa
siku ili kuwasaidia wananchi hasa wa eneo la Bweni kupata huduma hiyo
nyakati za usiku wanapohitaji kupata huduma za kijamii upande wa
Pangani.
MV.
Tanga ina uwezo wa kubeba tani 50 ambazo ni sawa na kubeba abiria 100
na magari 6 kwa pamoja. Uwezo wa MV. Tanga unalingana na uwezo wa kivuko
cha MV. Pangani II.
Imetolewa na,
Kitengo cha Habari na Mawasiliano TEMESA
0 comments:
Post a Comment