Na Godfriend Mbuya
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Godwin Gondwe amepiga
marufuku wananchi wa wilaya yake kucheza mchezo wa bao na ‘pool table’
wakati wa mchana ambapo ni muda wa kufanya kazi na kutekeleza falsafa ya
serikali ya awamu ya tano ya ‘Hapa Kazi Tu’
Gondwe ameyasema hayo alipofanya mazungumzo
maalumu na kipindi cha SUPAMIX kinachorushwa na kituo cha East Africa
Radio ambapo amesema baada ya kuteuliwa na Rais Magufuli na kuanza kazi
kuwa Mkuuu wa Wilaya hiyo alikuta muamkoa wa vijana katika kufanya kazi
ni mdogo huku wengi wakishinda vijiweni kwa kucheza pool table na bao
jambo ambalo amepiga marufuku wakati wa kazi.
“Nimekataza vijana kucheza michezo hiyo wakati wa kazi na nimewahamasisha kushiriki shughuli za ufugaji na kilimo ambapo wilaya ya Handeni inakubali sana kilimo
cha matunda, alizeti, ufuta na ufugaji wa mbuzi na kuku ambapo kwa
kushirikiana na idara ya ardhi tumekubaliana kutenga maeneo ya uwekezaji
kwa vijana ambapo serikali itawawezesha kuweza kuyafanyia kazi za
kilimo’’ Amesema Gondwe.
Aidha Mkuu huyio wa Wilaya amewataka vijana
kujiunga katika makundi ili waweze kupata fedha ambazo kila halmashauri
imetakiwa kutenga asilimia 5% ya mapato yake kwa ajili ya vijana na 5%
kwa ajili ya wanawake ili waweze kutumia mikopo watakayopata kujikwamua
kimaisha kwa kufanya shughuli mbalimbali.
0 comments:
Post a Comment