Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imewataka
wananchi wa Ukanda wa Pwani kuchukua tahadhari ya upepo mkali na mawimbi
makubwa ya Bahari ya Hindi kuanzia leo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TMA jana jijini Dar es Salaam,
ilieleza kuwapo upepo mkali unaozidi kasi ya kilomita 40 kwa saa na
mawimbi makubwa yanayozidi mita 2.0 kuanzia leo.
Ilitaja maeneo yatakayokubwa na dhahama hiyo ni mwambao wa mikoa ya
Tanga, Pwani (ikijumuisha Mafia), Dar es Salaam, Lindi na Mtwara pamoja
na visiwa vya Unguja na Pemba.
Mara kwa mara TMA imekuwa ikitoa tahadhari ya kuwapo kwa mvua,
upepo na mawimbi yasiyo ya kawaida na kuwataka wananchi wa maeneo husika
hasa wa mabondeni kuchukua tahadhari ikiwamo kuhama maeneo hatarishi.
Januari mwaka huu, TMA ilitoa tahadhari ya uwapo wa mvua nyingi ya
kiwango cha Tsunami na kuwataka wananchi wa mabondeni kuyahama makazi
yao.
Ilieleza mvua hizo zitaendelea hadi Machi mwaka huu, huku kukiwa na uwezekano mkubwa wa kutokeo tsunami.
Katika mvua zinazoendelea kunyesha nchini, baadhi ya mikoa ya Dar
es Salaam, Mwanza, Kagera, Geita na Tanga ilikumbwa na mafuriko
yaliyosababisha baadhi ya wananchi kupoteza maisha, kujeruhiwa pamoja na
mali kupotea.
Mapema Januari mwaka huu, serikali iliendesha ubomoji wa nyumba
zilizojengwa kwenye mto Msimbazi jijini, ikiwa ni wananchi wanaishi
bondeni na waliotakiwa kuhama.
Jumla ya nyumba 600 ziliwekwa alama ya X na 19,000 zilibomolewa na
serikali. Kwa sasa ubomoaji umesitishwa kutokana na kesi iliyofunguliwa
na wakazi zaidi ya 600 wa maeneo ya mabondeni kupinga ubomoaji huo.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment