Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mbunge wa Pangani (CCM), Jumaa Aweso, amefanya ziara katika Hospitali ya Wilaya ya Pangani na kukutana na upungufu kadhaa.
Ziara ya mbunge huyo hospitalini hapo, ilikuwa na lengo la kukagua
uwajibikaji wa watumishi pamoja na changamoto wanazokutana nazo.
Aweso baada kutembelea kila kitengo hospitalini hapo,
alieleza kutoridhishwa na huduma zinazotolewa katika na kwamba zina
upungufu mwingi ikilinganishwa na mategemeo ya wananchi kwa kuwa ndiyo
hospitali kubwa wilayani hapo.
Alitaja baadhi ya upungufu aliokutana nao ni pamoja na kutofanya
kazi kwa mashine ya x-ray na baadhi ya mashine za maabara, jengo la
upasuaji kuvuja na uhaba wa vifaa tiba.
Kutokana na hali hiyo, alisema atawasilisha kunakuhusika ili
serikali ichukue hatua za haraka kunusuru maisha ya wananchi wa wilaya
hiyo.
Aweso alieleza kushangazwa na uchakavu wa jengo la upasuaji hadi
kufikia hatua ya kuvuja pamoja na kukosekana kwa vifaa hivyo muhimu na
kudai kuwa hali hiyo licha ya kutishia maisha ya jamii, pia ni mzigo
kutokana na kulazimika kwenda mbali kufuata huduma hizo.
Mbunge huyo aliahidi kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya
kupitia mfuko wa jimbo kuhakikisha changamoto hizo zinapatiwa ufumbuzi
mara moja.
Kwa upande wake, aliahidi kuwashirikisha wadau mbalimbali wa
Pangani ili kuhakikisha kitengo cha upasuaji kinaimarishwa haraka ili
kupunguza kama si kumaliza kabisa tatizo la kukosekana kwa huduma hiyo.
Aweso alitumia fursa hiyo kuwaomba wananchi wa Pangani kujiunga
mfuko wa bima ya afya ili kupata matbabu kwa urahisi kwa kuwa kufanya
hivyo kutapunguza gharama kwa wananchi wengi ambao wengi wao hawana
uwezo wa kiuchumi.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment