Home » » PPF KUWAFIKISHA WAAJIRI MAHAKAMANI

PPF KUWAFIKISHA WAAJIRI MAHAKAMANI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

MFUKO wa pensheni wa PPF umesema utawafikisha mahakamani waajiri ambao hawapeleki michango kwa wakati kwani hali hiyo inasababisha usumbufu kwa wateja wao.
Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Meneja wa Kanda ya Kinondoni, Tanga na Pwani, Zahara Kayugwa wakati wa semina ya waajiri wa sekta mbalimbali jijini hapa.
Alisema hatua hiyo inaweza kusaidia waajiri kufikisha michango ya wafanyakazi wao kwa wakati.
“Kwa kweli inatubidi tuchukue hatua, kwa sababu unakuta mfanyakazi anakuja kudai mafao halafu mwajiri amechangia asilimia tano tu, sasa wateja wanatuona kama sisi ni wababaishaji… hatutawavumilia tena," alisema Kayugwa.
Aidha, akifungua semina hiyo Katibu Tawala Mkoa wa Tanga, Salim Chima, alisema Serikali inatambua na kuthamini mchango wa sekta ya hifadhi ya jamii nchini, hasa katika suala zima la kukuza na kuimarisha uchumi.

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa