Home » » WAHITIMU JKT WATAKIWA KUZINGATIA UTII

WAHITIMU JKT WATAKIWA KUZINGATIA UTII

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 

JESHI la Kujenga Taifa (JKT), limewataka wahitimu wa mafunzo ya awali kuzingatia utii na uwajibikaji katika jamii wanazoishi ili kuepuka migogoro.
Aidha, kupitia mafunzo waliyoyapata yasiwe kwa faida yao pekee bali kwa jamii nzima.
Wito huo umetolewa jana na Kanali Ferix Samillan, wakati wa ufungaji wa awali wa kundi la tatu la miaka 50 ya JKT kwa vijana waliomaliza kidato cha sita.
Kanali Samillan, alisema kuwa ni jukumu lao kuwalea vijana wa kitanzania, na kwamba vijana hao wamemaliza mafunzo yao ya awali takribani miezi mitatu, hivyo wako tayari kulitumikia Taifa lao huku wakiwa na uadilifu.
“Pia nawaasa kutokujiingiza katika makundi ambayo yanataka kuigawa nchi yetu, zingatieni uzalendo… Tanzania ni nchi yetu na hakuna ambaye ataipenda zaidi ya sisi wenyewe,” alisema KanaliSamillan.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Mrisho Gambo, ameitaka serikali kuandaa mpango maalumu kwa vijana hao ambao wamemaliza mafunzo, kwa kuwaandalia kitu ambacho kitawasaidia katika maisha yao baada ya kuhitimu.
Alisema kupitia mafunzo hayo, vijana hao watakuwa ni wa kipekee katika jamii zao hasa kwa wale wanaoona mafunzo haya hayana maana, kwani mtaani kuna maneno sana juu ya jambo hili.v
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa