Home » » CHADEMA WAJIPANGA KUMNG’OA MAJIMAREFU 2015

CHADEMA WAJIPANGA KUMNG’OA MAJIMAREFU 2015

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
CHAMA cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) kupitia kwa Mwenyekiti mpya wa Chama hicho wilayani Korogwe, Aulerian Nziku, amesema wamejipanga kumng’oa Mbunge wa Korogwe vijijini, Stephen Ngonyani, maarufu kama Profesa Majimarefu (CCM).
Akizungumza na Tanzania Daima juzi wilayani humo, Nziku ambaye ni Mjumbe wa Baraza Kuu la CHADEMA na Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa alisema, chama chake kitawahamasisha wananchi wa jimbo hilo ili kumg’oa Ngonyani kupitia sanduku la kura kutokana na kushindwa kusimamia maendeleo.
Nziku alisema kuwa mbunge huyo amekuwa akiwakumbatia madiwani wazembe ambao wameshindwa kuwatumikia wananchi ipasavyo na kuwa kero katika jimbo hilo .
“Hatuwezi kuendelea kushuhudia wananchi wakikosanishwa na viongozi na ndugu zao kwa imani za uganga badala ya kupelekewa maendeleo ya kiuchumi jimboni,” alisema.
Hata hivyo Nziku alisema Korogwe vijijini wamekosa mtetezi kwani fedha za mfuko wa jimbo hazifahamiki namna zinavyotumika, akitolea mfano msaada wa fedha zilizotolewa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, (UNDP) sh Mil. 253/-, ambazo hazieleweki zimefanya kazi gani.
Nziku alisema baadhi ya viongozi wamekuwa wakiuza ardhi ya wananchi na kuwasababishia kuwa maskini.
Akizungumzia tuhuma hizo, Ngonyani alimtaka Nziku kwaweka wazi madiwani ambao amewakumbatia kwani amejitaidi kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa wakati
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa