Home » » SURVEY YANG'ARA MICHUANO YA NANENANE TANGA

SURVEY YANG'ARA MICHUANO YA NANENANE TANGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Timu ya Survey Veterani ya jijini Dar es Salaam imeifunga timu ya Kombaini Vijana ya jijini Tanga kwa mabao 2-1, katika mchezo wa kuazimisha Siku ya Wakulima (Nanenane) kwenye viwanja vya Disuza, vilivyopo mkoani hapa.

Mchezo huo ambao ulidhaminiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), ulikuwa na lengo la kukutanisha timu za maveterani ili kujenga mshikamano na kuhamasisha watu kupenda michezo nchini.
Katika mchezo huo, mchezaji wa Survey, Carlos Mdinga alijifunga wakati akijaribu kuokoa mpira uliopigwa na wapinzani hatua ambayo ilisababisha kuzaa bao dakika ya pili.
Hata hivyo katika mchezo huo timu ya Survey ilionyesha makali yake, kwani dakika ya 40 walisawazisha bao hilo kupitia kwa kiungo wake, Silyvester Malango.
Bahati ilizidi kung’aa kwa timu ya Survey Veterani baada ya kupata bao la pili dakika ya 70, lililowekwa wavuni na mshambuliaji David Emmanuel na hivyo kuibuka na ushini wa mabao 2-1.
Katika mchezo mwengine, Best point veterani iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya kombaini ya wazee ya jijini Tanga.
Mabao ya Best Point yalifungwa na Sadiki Salumu (7) na Miraji Paulo katika dakika za mwisho za mchezo huo.
Baada yakumalizika kwa mchezo huo, kocha Seleman Mgaya, ambaye ni Katibu wa Survey Veterani ya Dar es Salaam, alisema wamefurahishwa na ushirikiano unaotolewa na mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF) hasa kwa kuonyesha mchango wao katika michezo.
“Tunaishukuru NSSF kwa moyo wa kutukutanisha pamoja kimichezo, hatua ambayo tunajivunia kwani wao wametambua umuhimu wetu, hivyo hatuna budi kutoa ushirikiano,” alisema Mgaya.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa