Home » » MLINGANO WAPATA KITUO CHA AFYA

MLINGANO WAPATA KITUO CHA AFYA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
SHIRIKA la Kikorea la kuhudumia afya za watoto chini ya miaka kumi (UHIC), kupitia mradi wake wa Keeper, limefungua kituo cha afya katika Kijiji cha Mlingano, Muheza mkoani Tanga.
Akizungumza katika hafla ya ufunguzi, Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu, alisema kituo hicho kitasaidia kwa kiasi kikubwa wananchi wa eneo hilo kutibu watoto wao kwa haraka pindi wanapopatwa na maradhi mbalimbali.
Alisema nia ya serikali ni kuhakikisha wananchi wake hawatembei umbali mrefu kufuata huduma za kijamii ikiwemo vituo vya afya, hivyo uamuzi wa kuweka kituo eneo hilo ni wa busara na utawapunguzia wananchi kwenda umbali mrefu kufuata huduma hiyo.
“Niwapongeze UHIC kupitia Shirika la Kimaendeleo la Korea ya Kusini (Koica), kwa kuweza kubuni mradi huu wa kutoa tiba kwa watoto wenye umri chini ya miaka 10, utasaidia kuboresha afya za watoto wengi kwenye wilaya hii, hasa wale wanaoishi maeneo ya vijijini,” alisema Mgalu.
Kwa upande wake, Mwakilishi Mkazi wa Koica, Kim Seung Bum, alisema kuwa afya bora kwa mtoto chini ya miaka kumi ni muhimu katika kujiletea maendeleo endelevu kwa ngazi ya familia na taifa kwa ujumla.
Mwenyekiti wa kijiji hicho, Rashid Iddi, aliiomba serikali kuharakisha kupeleka huduma ya umeme kwenye kituo hicho ili kiweze kutoa huduma muda wote badala ya sasa ikifika jioni hulazimika kufungwa
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa