Home » » ATAKA ELIMU YA UJASIRIAMALI WA VIKUNDI

ATAKA ELIMU YA UJASIRIAMALI WA VIKUNDI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
SERIKALI imetakiwa kuvipa  kipaumbele  vikundi vya ujasiriamali ikiwa na pamoja na kuwapatia elimu ya mafunzo mara kwa mara.
 Ushauri huo ulitolewa na Mwalimu wa Vikoba, Rukia Mwinyi wakati wa mafunzo ya wajasiliamali yaliyofanyika jana jijini Tanga, akisema kuwa endapo serikali itaweza kutoa elimu hiyo ipasavyo ile sera ya kupambana na umasikini itafanikiwa.
 “Jambo hili likifuatiliwa kwa umakini tutafanikiwa kujikomboa katika umasikini kwani wajasiriamali waliowengi hasa katika vikundi vyetu hatuna elimu hii kwa ufasaha ambayo tunaihitaji kwa nguvu zote,”alisema Rukia.
 Aidha, Rukia alisema mafunzo kwa wajasiriamali yamekuwa hayatolewi mara kwa mara kitendo kinachowafanya kutokuwa na uelewa sahihi juu ya suala hilo na kushindwa kutimiza malengo waliokusudia.
 Awali akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Dendego aliwataka kuwa na uchungu na maendeleo ikiwa ni pamoja na kutangaza fursa za kimaendeleo wanazozifanya ili kufikia lengo la kuongeza pato la mtu mmoja mmoja.
 Dendego alisema mbali na kutangaza bidhaa zao pia wajikite katika shughuli za kilimo ambazo wataziuza nje ya nchi hususani Kenya ambako wamekuwa na uhitaji mkubwa wa mazao kama chakula yatayopatikana mkoani Tanga.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa