Home » » VIONGOZI KILINDI MBARONI WAKIDAIWA KUSHAWISHI MAPIGANO

VIONGOZI KILINDI MBARONI WAKIDAIWA KUSHAWISHI MAPIGANO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MWENYEKITI wa Serikali ya Kijiji cha Kibirashi, wilayani Kilindi, Yussuph Mwegango na viongozi wenzake wanne wa ngazi ya vitongoji, vijiji, kata na tarafa wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kushawishi mapigano kati ya wakulima na wafugaji ambayo yalisababisha vifo vya watu wawili.
Wiki iliyopita watu wanane walijeruhiwa vibaya huku wawili kati yao wakipigwa risasi na polisi kutokana na mapigano ya kugombea ardhi wilayani Kilindi.
Mapigano hayo yalisababisha wakulima kuteka Kijiji cha Kiberashi kwa kutumia silaha baridi kisha kuvunja nyumba mbili za kisasa, kuteketeza pikipiki nne na baadaye kupora mali katika maduka ya wafanyabiashara wa jamii ya wafugaji.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Selemani Liwowa, aliwataja viongozi wengine kuwa ni Salim Rajab (Mwenyekiti Kitongoji cha Kibirashi), Ayoub Hajji (Mjumbe wa Serikli ya Kijiji cha Kibirashi) na Zubeir Machaku (Ofisa Mtendaji Kijiji cha Kibirashi).
“Kwa sasa hali ni shwari kutokana na kuongeza nguvu za kiusalama kwani askari kutoka wilaya za Kilindi, Handeni na Tanga wameweka kambi maalumu ya ulinzi katika kijiji hicho ili kuhakikisha hali inarudi
kuwa ya usalama,” alisema.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

Post a Comment

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Tanga Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa